Isaiah 3:4-9
4 aNitawafanya wavulana wawe maafisa wao,
watoto ndio watakaowatawala.
5 bWatu wataoneana wao kwa wao:
mtu dhidi ya mtu, na jirani dhidi ya jirani yake.
Kijana atainuka dhidi ya mzee,
mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.
6 Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake
katika nyumba ya baba yake na kusema,
“Unalo joho, sasa uwe kiongozi wetu,
tawala lundo hili la magofu!”
7 cLakini siku hiyo atapiga kelele akisema,
“Sina uponyaji.
Sina chakula wala mavazi katika nyumba yangu,
msinifanye niwe kiongozi wa watu.”
8 dYerusalemu inapepesuka,
Yuda inaanguka;
maneno yao na matendo yao ni kinyume na Bwana,
wakiudharau uwepo wake uliotukuka.
9 eNyuso zao zinavyoonekana zinashuhudia dhidi yao,
hujivunia dhambi yao kama Sodoma,
wala hawaifichi.
Ole wao!
Wamejiletea maafa juu yao wenyewe.
Copyright information for
SwhKC